Siku ya jana alipokuwa akizungumza na watumishi wa
Halmashauri za wilaya ya Mbeya na Halmashauri ya Jiji la Mbeya katika
mkutano uliofanyika ukumbi wa Benjamin Mkapa waziri mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amemuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mbeya, Emanuel Kiabo kumkamata na
kumuhoji aliyekuwa Meya wa Jiji la Mbeya Atanas Kapunga na wenzake 11 kwa tuhuma za kuisababishia Serikali hasara ya sh. bilioni 63.448.
“Serikali hii haiwezi ikawaacha watu hawa ambao wameisababishia hasara kubwa kiasi hiki tena kwa halmashauri moja. Kama wako humu ndani naagiza wakamatwe na waanze kuhojiwa na ambao wamestaafu au kuhamishwa kituo cha kazi wasakwe popote walipo ili nao waje kuhojiwa,” aliagiza waziri mkuu.
“Serikali hii haiwezi ikawaacha watu hawa ambao wameisababishia hasara kubwa kiasi hiki tena kwa halmashauri moja. Kama wako humu ndani naagiza wakamatwe na waanze kuhojiwa na ambao wamestaafu au kuhamishwa kituo cha kazi wasakwe popote walipo ili nao waje kuhojiwa,” aliagiza waziri mkuu.
0 comments:
Post a Comment