Wednesday, April 5, 2017

Mbowe awatuhumu JPM na Majaliwa kwa kuhusika kutochaguliwa wabunge wa upinzani bunge la Afrika Mashariki.

Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Freeman Mbowe amtuhumu Rais John Magufuli pamoja na waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusika  na  alichodai kuwa ni kukiukwa kwa taratibu za uchaguzi wa kuwapata wawakilishi katika bnge la afrika mashariki
 Mbowe ameongea hayo jana usiku mara baada ya kutoka kwenye ukumbi wa bunge  ambapo amedai kuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Rais Magufuli kuhusika kwenye mchakato wa kuyakataa majin ya wagombea wa Chadema.

Mbowe amesema  kuwa, wao hawatakubaliana na hilo kwa sababu Spika wa Bunge amekiuka kanuni za bunge, na uchaguzi wote ulikuwa wa kasoro.
Wagombea waliopendekezwa na Chadema  Wenje Na Masha ambao walipigiwa  kura za hapana katika  kuwania kuiwakilisha Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki. Nje ya ukumbi wa Bunge Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe ameongea na waandishi wa habari na kusema kuwa hawakubaliani na matokeo na watakwenda Mahakamani kudai haki yao.
 













Share:

0 comments:

Post a Comment

Breaking News

Contact Us

Name

Email *

Message *

Translate

Total Pageviews