Wednesday, March 1, 2017

Polisi wajiweka kando sakata la majina 65 ya makonda.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limejiweka kando kuhusu sakata la majina 65 ya watu waliyotajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akiwatuhumu kujihusisha na dawa za kulevya.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini jana, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, alipoulizwa kuhusu mwitikio wa wahusika kwenda polisi kama walivyotakiwa na Makonda, alisema suala hilo sasa haliko chini yake.

Alisema tayari walishakabidhi majina ya watuhumiwa kwenye ofisi ya Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya baada ya Rais John Magufuli kumteua Kamishna Mkuu, Rogers Sianga kuiongoza.

Kamishna Sirro alisema wanawashikiliwa watuhumiwa 105 wa dawa za kulevya ikiwamo bangi na pombe ya gongo. Alisema katika msako wao wamekamata dawa za kulevya kete 413 (bila kutaja ni aina gani), puli 50, misokoto ya bangi 86 na gongo lita 45.


Awamu ya tatu ya vita ya Makonda dhidi ya dawa za kulevya inahusisha majina 97 ya watu ambao hayakutajwa hadharani na Mkuu huyo wa Mkoa badala yake aliyakabidhi kwa Kamishna Sianga Februari 13 kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Source. Muungwana.blogspot
Share:

0 comments:

Post a Comment

Breaking News

Contact Us

Name

Email *

Message *

Translate

Total Pageviews